Ratiba ya Mitihani ya Kidato cha Sita (ACSEE) Mei 2026, Ratiba ya Kidato cha Sita 2026, NECTA ACSEE Timetable 2026 PDF, Ratiba ya NECTA Mei 2026, Mitihani ya Kidato cha Sita 2026.
Baraza la Mitihani la Tanzania (NECTA) limetoa ratiba rasmi ya mtihani wa Kidato cha Sita (Advanced Certificate of Secondary Education Examination – ACSEE) kwa mwaka 2026. Kwa mujibu wa ratiba hiyo, mitihani inatarajiwa kuanza rasmi tarehe 04 Mei, 2026 na kukamilika mwishoni mwa mwezi Mei.
Maandalizi ya mitihani ya vitendo (practicals) yataanza mapema tarehe 14/05/2026 kwa masomo ya Physical Education.
Mchanganuo wa Masomo na Tarehe za Mitihani (Wiki ya Kwanza)
| Siku na Tarehe | Kipindi cha Asubuhi (8:00 AM – 11:00 AM) | Kipindi cha Mchana (2:00 PM – 5:00 PM) |
| Jumatatu 04/05/2026 |
General Studies |
History 1, Biology 1, Accountancy 1, Chinese 1 |
| Jumanne 05/05/2026 |
Kiswahili 1, Physics 1, Agriculture 1, Commerce 1, Food & Nutrition 1 |
Geography 1, Physical Education 1, French 1, Education |
| Jumatano 06/05/2026 |
Kiswahili 2, Basic Applied Mathematics, Advanced Mathematics 1 |
English Language 1, Chemistry 1, Economics 1 |
| Alhamisi 07/05/2026 |
Geography 2, Agriculture 2, Accountancy 2, Food & Nutrition 2 |
Fine Art 1, Chinese 2, Physics 2, Economics 2 |
| Ijumaa 08/05/2026 |
History 2, Biology 2 |
English Language 2, Chemistry 2, Commerce 2 |
Mitihani ya Vitendo (Practicals) – Wiki ya Pili na Tatu
Ratiba inaonyesha msisitizo mkubwa kwenye mitihani ya vitendo kuanzia katikati ya mwezi Mei:
-
Jumatatu 11/05/2026: Advanced Mathematics 2 na Agriculture 3 (Practical).
-
Jumanne 12/05/2026: Fine Art 2 na Biology 3A (Practical).
-
Jumatano 13/05/2026: Chemistry 3A (Practical).
-
Alhamisi 14/05/2026: Physics 3A (Practical).
-
Wiki ya Mwisho (18/05/2026 – 25/05/2026): Imepangwa kwa ajili ya Biology, Chemistry, na Physics (Practical) kwa vikundi B na C.
Kanuni na Maelekezo kwa Watahiniwa
Baraza la Mitihani limetoa angalizo kwa watahiniwa wote kuzingatia mambo yafuatayo:
-
Muda: Watahiniwa wanapaswa kufika chumba cha mtihani mapema. Mwanafunzi atakayechelewa kwa zaidi ya dakika 30 hataruhusiwa kufanya mtihani.
-
Udanganyifu: Ni marufuku kuingia na simu au maandishi yoyote kwenye chumba cha mtihani. Atakayegundulika kufanya udanganyifu atafutiwa matokeo.
-
Siku za Mapumziko: Mitihani itaendelea kama ilivyopangwa hata kama kutatokea siku ya mapumziko ya kitaifa (Public Holiday).
-
Watahiniwa Binafsi: Lazima wawe na barua ya utambulisho inayowaruhusu kufanya mtihani katika kituo husika.
Pakua Ratiba ya ACSEE 2026 (PDF File)
Unaweza kupakua nakala rasmi ya ratiba hii ya NECTA kwa ajili ya kumbukumbu na maandalizi yako kupitia link iliyopo hapa chini:

DOWNLOAD PDF HAPA: RATIBA YA KIDATO CHA SITA 2026
